Tuesday, 17 November 2015

PONGEZI KWA SPIKA MTEULE MP, MBUNGE WA JIMBO LA KONGWA MHE JOB NDUGAI


                                   Spika wa bunge 11, Mhe Job Ndugai(mbunge wa Kongwa)
Chama Cha Mapinduzi tawi la Moscow-Urusi tunayo furaha kubwa kupokea ushindi uliotukuka wa Mhe Job Ndugai kwa kuchaguliwa kuwa spika wa bunge la 11 la jamuhuri ya muungano wa Tanzania.
Uongozi wa tawi unapenda kuchukua fursa hii ya kipekee kuwashukuru wabunge wa CCM kwa kuungana kwa pamoja, kuwa na imani na kumpigia kura nyingi Mhe Job Ndugai, ushindi wa Mhe Ndugai ni ushindi wa watanzania kwani Mhe Ndugai ni kiongozi jasiri, mwadilifu,mchapakazi, anayependa watu na anayependwa na watu hivyo tunaamini atawatendea haki watanzania kupitia muhimili huo muhimu wa serikali.
Katika taarifa yake fupi, mwenyekiti wa tawi Ndg Salim Mfungahema alisema anafahamu vizuri pasi na mashaka utendaji na uwajibikaji ulio bora wa Mhe Ndugai kwani aliwahi kufanyanae kazi ya kuimarisha chama  katika jimbo la Kongwa mwaka 2012. Kupitia ziara iyo ya wiki moja jimboni kongwa Ndg Mfungahema anasema alijifunza mambo mengi kupitia mwanasiasa huyo mkongwe na anayekubalika sana jimboni kwake, hivyo anaamini CCM imefanya chaguo sahihi na tunaamini ataongoza vema muhimili huo wa kutunga sheria na kusimamia serikali.

Kidumu Chama Chama Mapinduzi,
Imetolewa na katibu wa tawi,
Ndg Hassan Kapilima.
Trh 17.11.2015.

Thursday, 5 November 2015

RAIS DKT JOHN P MAGUFULI KULA KIAPO LEO, KIKWETE KUSTAAFU RASMI.


Rais wa awamu ya tano Dkt John P Magufuli

Leo tarehe 5 mwezi wa 11, 2015. Tanzania imeandika historia nyingine mpya kwa kupata Rais mpya wa awamu ya tano.
Chama Cha Mapinduzi tawi la CCM Moscow Urusi tunayo furaha kubwa kushuhudia jinsi raisi wa awamu ya nne na rais wa awamu ya tano walivyoweza kubadilishana madaraka katika misingi ya amani, upendo na kuheshimu katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania, aidha uongozi wa tawi tunajivunia taswira ya kipekee ya mfumo wa uongozi ndani ya taifa letu, misingi ambayo imejengwa kikamilifu na TANU na ASP, na badae CCM.
                                       Rais Mhe, Dkt John Pombe Magufuli akila kiapo

Uongozi unapenda kuchukua fursa hii ya kipekee kumpongeza rais wa awamu ya tano Dtk John P Magufuli kwa kula kiapo cha uaminifu, uadilifu, kuilinda na kuitetea katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania. Mbali na pongezi hizo uongozi unaamini rais wa awamu ya tano ni mchapa kazi, mwadilifu, kiongozi hodali na mwenye msimamo thabiti, hivyo tunaamini ndoto za watanzania zitatimia, kwa kufanya hivyo atakuwa amewatendea haki watanzania, pia atakuwa amekipa heshima chama chake CCM na kukihakikishia ushindi daima.

                        KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
                        IMETOLEWA NA MWENYEKITI WA TAWI.
                        SALIM .A. MFUNGAHEMA

Friday, 30 October 2015

CCM-MOSCOW-URUSI YAMPONGEZA RAIS MTEULE WA AWAMU YA 5 DR JOHN POMBE MAGUFULI

    Chama cha mapinduzi tawi la CCM-Moscow Urusi tumepokea kwa furaha kubwa ushindi wa CCM katika nafasi mbalimbali, Urais, ubunge na udiwani.
Aidha Uongozi wa CCM Moscow unapenda kuchukua nafasi hii ya kipekee kumpongeza rais mteule wa awamu ya 5 wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli kwakuchaguliwa na watanzania kwa kura nyingi zilizompa ushindi mkubwa na kukipatia chama cha mapinduzi ushindi kishindo, aidha ushindi wa Dr Magufuli umedhihirisha wazi CCM  ni chama bora, imara chenye nguvu na ni chama ambacho ilani yake inatekelezeka.
       Pia tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa rais anayemaliza muda wake Dr Jakaya Kikwete kwa kumaliza muda wake wa kuliongoza taifa la Tanzania miaka 10, kwa mafanikio makubwa na iyo ndio siri ya ushindi wa CCM.
        Pongezi nyingi ziwaendee marais wastaafu mzee Ally Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa, viongozi wa CCM kuanzia ngazi ya shina hadi taifa, wanachama wa CCM, na watanzania wote kwa ujumla bila kujali itikadi ya vyama vyao, kwa kuendelea kuwa na imani na CCM, kuichagua na kuipa ridhaa ya kuongoza dola.


                                    Mungu ibariki Tanzania,
                                    Mungu ibariki Afrika,
                                    Mungu ibariki CCM Daima.
                                    Kidumu Chama Cha Mapinduzi.
                       Imetolewa na mwenyekiti wa tawi ndg Salim A. Mfungahema 

Thursday, 9 October 2014







Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dk Jakaya Mrisho Kikwete na rais wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar Dk Ally Mohamed Shein wamekabidhiwa katiba iliyopendekezwa na bunge maalum la katiba ikiwa ni hatua muhimu katika historia ya Tanzania kuelekea kupata katiba mpya ambayo kwa mara ya kwanza imehusisha maoni ya wananchi, makundi maalum, taasisi wanasiasa na viongozi mbalimbali tangu taifa kupata uhuru wake.

Majira ya saa sita na nusu mchana ndipo makundi mbalimbali ya wageni waalikwa, viongozi wa juu wa serikali mabalozi marais na mawaziri wa kuu wastaafu wakaingia katika viwanja vya jamuhuri na kisha majira ya saa tisa na nusu rais wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar Dk Ally Mohamed Shein akawasili na kufuatiwa na rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania. 


Mara baada ya itifaki ya uongozi kuwasili shughuli ikaanza rasmi ambapo mwenyekiti wa kamati ya uandishi ya bunge maalum Mhe Adrew Chenge akaelezea maudhui ya katiba iliyopendekezwa pamoja na mambo mengine akasema katiba hiyo ina jumla ya sura 19 na ibara 296 na nyongeza tatu ambapo rasimu ya awali iliyowasilishwa bungeni ilikuwa na sura 17 na ibara 211 huku suala la muundo wa serikali likisalia kuwa serikali mbili.

Friday, 6 June 2014

MWENYEKITI CCM TAWI LA MOSCOW URUSI ATOA MSIMAMO WAKE JUU YA MCHAKATO WA KATIBA, ASEMA SERIKALI MBILI NDIO SULUHISHO.

   
MWENYEKITI TAWI LA CCM MOSCOW URUSI, NDG SALIM MFUNGAHEMA:  



 Mwenyekiti tawi la CCM Moscow Ndg Mfungahema Salim amesema muundo wa muungano wa serikali Mbili ndio suluhisho pekee la watanzania, Akizungumza katika kamati ya siasa ya tawi bwana Mfungahema alisema muungano wa serikali mbili ndio umetufikisha hapa tulipo na kuna mafanikio makubwa TULIYOYAPATA, pamoja na changamoto chache zinazojitokeza lakini zinarekebishika.

 Bwana Mfungahema aliwataka vijana wa CCM kuendelea kuungamkono muungano wa serikali mbili kwani ndio muungano wenye tija kwa taifa. Bwana Mfungahema alisema serikali tatu ni mzigo kwa taifa na hivyo hatunabudi kuendelea na mfumo wa serikali mbili na ikibidi tuelekee kwenye serikali moja kwani ni muungano sahihi na utaleta tija na mshikamano zaidi kwa watanzania. Pia mwenyekiti alimshukuru Mh Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dr Jakaya Mrisho Kikwete kwa jitiada zake za kuwaletea maendeleo watanzania na kuboresha utawala bora Tanzania na Afrika kwa ujumla.
 Mh mwenyekiti Ndg SalimMfungahema alitumia fursa hiyo pia kumpongeza Mh Rais Kikwete kwa kupata tunzo la kuwa kiongozi bora barani Afrika mwenye mchango mkubwa wa kuleta maendeleo, amani na utawala bora, bwana Mfungahema alisema Rais Kikwete ametupatia heshima kubwa watanzania kote duniani.
   Kuhusu uchaguzi wa mwaka 2015, bwana Mfungahema alisema CCM inatarajia kupata ushindi mkubwa na wa kishindo mwaka 2015 kwa sababu CCM imetekeleza ilani yake ya uchaguzi vizuri na kwa wakati, na hivyo kuwafanya wananchi wawe na imani kubwa na CCM.

   Mwenyekiti pia alimpongeza katibu mkuu wa CCM MH Abdulrahmani Kinana kwa mchango wake mkuwa na kuimalisha chama, na kukipa cha uhai mkubwa na kurudisha imani ya wananchi kwa CCM, alisema jukumu la kuimalisha chama ni la kila mwana CCM na sio viongozi pekee, hivyo alitoa wito kwa vijana wanaporudi nyumbani Tanzania kutoa ushirikiano wa kuimarisha chama katika maeneo yao, ikiwa ni pamoja na kuelezea jinsi ilani inavyotekelezeka.

                                KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
                               IMETOLEWA NA KATIBU WA TAWI
                              NDG HASSANI KAPILIMA, CCM MOSCOW.